Agano la Kale

Agano Jipya

Yohane 5:44-47 Biblia Habari Njema (BHN)

44. Mwawezaje kuamini, hali nyinyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu nyinyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu?

45. Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye nyinyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki.

46. Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia, maana Mose aliandika juu yangu.

47. Lakini hamyaamini yale aliyoandika; mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?”

Kusoma sura kamili Yohane 5