Agano la Kale

Agano Jipya

Yohane 1:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hapo mwanzo, Neno alikuwako; naye alikuwa na Mungu, naye alikuwa Mungu.

2. Tangu mwanzo Neno alikuwa na Mungu.

3. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa; hakuna hata kiumbe kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.

4. Yeye alikuwa chanzo cha uhai na uhai huo ulikuwa mwanga wa watu.

5. Na mwanga huo huangaza gizani, nalo giza halikuweza kuushinda.

6. Mungu alimtuma mtu mmoja jina lake Yohane,

Kusoma sura kamili Yohane 1