Agano la Kale

Agano Jipya

Yakobo 3:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Hekima ya namna hiyo haitoki juu mbinguni; hekima hiyo ni ya ulimwengu, na ya kidunia, tena ni ya kishetani.

16. Maana popote palipo na wivu na ubinafsi, hapo pana fujo na kila aina ya uovu.

17. Lakini hekima itokayo juu mbinguni, kwanza ni safi; inapenda amani, upole na huwajali watu; imejaa huruma na huzaa matunda ya matendo mema; haina ubaguzi wala unafiki.

18. Uadilifu ni mazao ya mbegu ambazo wapenda amani hupanda katika amani.

Kusoma sura kamili Yakobo 3