Agano la Kale

Agano Jipya

Yakobo 2:9-16 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo sheria inawahukumu nyinyi kuwa mna hatia.

10. Anayevunja amri mojawapo ya sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja sheria yote.

11. Maana yuleyule aliyesema: “Usizini,” alisema pia “Usiue.” Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini, lakini umeua, wewe umeivunja sheria.

12. Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.

13. Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.

14. Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?

15. Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.

16. Yafaa kitu gani nyinyi kuwaambia hao: “Nendeni salama mkaote moto na kushiba,” bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?

Kusoma sura kamili Yakobo 2