Agano la Kale

Agano Jipya

Yakobo 2:23-26 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: “Abrahamu alimwamini Mungu, na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki ya Mungu.”

24. Mnaona, basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake, na si kwa imani peke yake.

25. Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.

26. Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.

Kusoma sura kamili Yakobo 2