Agano la Kale

Agano Jipya

Yakobo 2:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.

20. Mpumbavu wee! Je, wataka kuoneshwa kwamba imani bila matendo imekufa?

21. Je, Abrahamu babu yetu alipataje kukubaliwa kuwa mwadilifu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa tambiko mwanawe Isaka juu ya madhabahu.

22. Waona, basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.

Kusoma sura kamili Yakobo 2