Agano la Kale

Agano Jipya

Yakobo 2:13-17 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.

14. Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?

15. Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.

16. Yafaa kitu gani nyinyi kuwaambia hao: “Nendeni salama mkaote moto na kushiba,” bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?

17. Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.

Kusoma sura kamili Yakobo 2