Agano la Kale

Agano Jipya

Waroma 4:19-25 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Alikuwa mzee wa karibu miaka 100, lakini imani yake haikufifia ingawa alijua kwamba mwili wake ulikuwa kama umekufa, na pia mkewe, Sara, alikuwa tasa.

20. Abrahamu hakuionea mashaka ile ahadi ya Mungu; alipata nguvu kutokana na imani, akamtukuza Mungu.

21. Alijua kwamba Mungu anaweza kuyatekeleza yale aliyoahidi.

22. Ndiyo maana Mungu alimkubali kuwa mwadilifu.

23. Inaposemwa, “Alimkubali,” haisemwi kwa ajili yake mwenyewe tu.

24. Jambo hili linatuhusu sisi pia ambao tunamwamini Mungu aliyemfufua Yesu, Bwana wetu, kutoka kwa wafu.

25. Yeye alitolewa auawe kwa ajili ya dhambi zetu, akafufuka ili tufanywe waadilifu.

Kusoma sura kamili Waroma 4