Agano la Kale

Agano Jipya

Waroma 3:2-13 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Naam, iko faida kwa kila upande. Kwanza, Mungu aliwakabidhi Wayahudi ujumbe wake.

3. Lakini itakuwaje iwapo baadhi yao hawakuwa waaminifu? Je, jambo hilo litaondoa uaminifu wa Mungu?

4. Hata kidogo! Mungu hubaki mwaminifu daima, ingawaje kila binadamu ni mwongo. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:“Kila usemapo,maneno yako ni ya kweli;na katika hukumu,wewe hushinda.”

5. Lakini, ikiwa uovu wetu unathibitisha kwamba Mungu anatenda kwa haki, tutasema nini? Je, tutasema kwamba anakosa haki akituadhibu? (Hapa naongea kibinadamu).

6. Hata kidogo! Ingekuwa hivyo, Mungu angewezaje kuuhukumu ulimwengu?

7. Labda utasema: “Ikiwa ukosefu wa uaminifu kwa upande wangu unamdhihirisha Mungu kuwa mwaminifu zaidi na hivyo kumpatia utukufu, basi singepaswa kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!”

8. Ni sawa na kusema: Tufanye maovu ili tupate mema! Ndivyo wengine walivyotukashifu kwa kutushtaki kwamba tumefundisha hivyo. Watahukumiwa wanavyostahili!

9. Tuseme nini, basi? Je, sisi Wayahudi ni bora kuliko wengine? Hata kidogo! Kwa maana nimekwisha bainisha hapo mwanzoni kwamba Wayahudi na watu wa mataifa mengine wote wako chini ya utawala wa dhambi.

10. Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:“Hakuna hata mmoja aliye mwadilifu!

11. Hakuna mtu anayeelewa,wala anayemtafuta Mungu.

12. Wote wamepotokawote wamekosa;hakuna atendaye mema,hakuna hata mmoja.

13. Makoo yao ni kama kaburi wazi,ndimi zao zimejaa udanganyifu,midomoni mwao mwatoka maneno yenye sumu kama ya nyoka.

Kusoma sura kamili Waroma 3