Agano la Kale

Agano Jipya

Waroma 14:11-21 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Maana Maandiko yanasema:“Kama niishivyo, asema Bwana,kila mtu atanipigia magoti,na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”

12. Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja juu yake mwenyewe mbele ya Mungu.

13. Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu au kumsababisha aanguke katika dhambi.

14. Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.

15. Kama ukimhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, basi mwenendo wako hauongozwi na upendo. Usikubali hata kidogo chakula chako kiwe sababu ya kupotea kwa mtu mwingine ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake!

16. Basi, msikubali kitu mnachokiona kwenu kuwa chema kidharauliwe.

17. Maana ufalme wa Mungu si shauri la kula na kunywa, bali unahusika na kuwa na uadilifu, amani na furaha iletwayo na Roho Mtakatifu.

18. Anayemtumikia Kristo namna hiyo humpendeza Mungu, na kukubaliwa na watu.

19. Kwa hiyo tuyazingatie daima mambo yenye kuleta amani, na yanayotusaidia kujengana.

20. Basi, usiiharibu kazi ya Mungu kwa sababu ya ubishi juu ya chakula. Vyakula vyote ni halali, lakini haifai kula chakula ambacho kitamfanya mtu aanguke katika dhambi.

21. Afadhali kuacha kula nyama, kunywa divai, au kufanya chochote ambacho chaweza kumsababisha ndugu yako aanguke.

Kusoma sura kamili Waroma 14