Agano la Kale

Agano Jipya

Waroma 14:10-14 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Kwa nini basi, wewe wamhukumu ndugu yako? Nawe, kwa nini wamdharau ndugu yako? Sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.

11. Maana Maandiko yanasema:“Kama niishivyo, asema Bwana,kila mtu atanipigia magoti,na kila mmoja atakiri kwamba mimi ni Mungu.”

12. Kwa hiyo, kila mmoja wetu atatoa hoja juu yake mwenyewe mbele ya Mungu.

13. Basi, tuache kuhukumiana, bali tuazimie kutokuwa kamwe kikwazo kwa ndugu au kumsababisha aanguke katika dhambi.

14. Katika kuungana na Bwana Yesu, nina hakika kwamba hakuna kitu chochote kilicho najisi kwa asili yake; lakini, mtu akidhani kwamba kitu fulani ni najisi, basi, kwake huwa najisi.

Kusoma sura kamili Waroma 14