Agano la Kale

Agano Jipya

Wakolosai 4:14-18 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.

15. Salamu zetu kwa ndugu wa Laodikea. Msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.

16. Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na nyinyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata wao.

17. Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.

18. Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.

Kusoma sura kamili Wakolosai 4