Agano la Kale

Agano Jipya

Wakolosai 4:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.

2. Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.

3. Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.

4. Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.

5. Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri wakati mlio nao.

Kusoma sura kamili Wakolosai 4