Agano la Kale

Agano Jipya

Wakolosai 3:4-7 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Uhai wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.

5. Basi, ueni chochote kilicho ndani yenu ambacho ni cha kidunia: Uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).

6. Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.

7. Wakati mmoja nyinyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.

Kusoma sura kamili Wakolosai 3