Agano la Kale

Agano Jipya

Wakolosai 3:17-23 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.

18. Enyi wake, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.

19. Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.

20. Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.

21. Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.

22. Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.

23. Kila mfanyacho, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.

Kusoma sura kamili Wakolosai 3