Agano la Kale

Agano Jipya

Wakolosai 3:15-20 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo nyinyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!

16. Ujumbe wa Kristo na ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.

17. Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.

18. Enyi wake, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.

19. Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.

20. Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.

Kusoma sura kamili Wakolosai 3