Agano la Kale

Agano Jipya

Wagalatia 5:20-26 Biblia Habari Njema (BHN)

20. kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, choyo, mabishano, mafarakano;

21. husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine kama hayo. Nawaambieni tena kama nilivyokwisha sema: Watu wanaotenda mambo hayo hawataupata ufalme wa Mungu uwe wao.

22. Lakini matokeo ya kuongozwa na Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu,

23. upole na kiasi. Hakuna sheria inayoweza kupinga mambo hayo.

24. Wale walio na Kristo wameisulubisha hali yao ya kidunia pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.

25. Tukiishi kwa msaada wa Roho, na tuufuate mwongozo wake.

26. Basi, tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.

Kusoma sura kamili Wagalatia 5