Agano la Kale

Agano Jipya

Wagalatia 5:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kristo alitupa uhuru, akataka tubaki huru. Basi, simameni imara wala msikubali tena kuwa chini ya nira ya utumwa.

2. Sikilizeni! Ni mimi Paulo ninayesema nanyi! Kama mkikubali kutahiriwa, Kristo hatawafaidia chochote.

3. Nasema tena wazi: Kila anayekubali kutahiriwa itambidi kuishika sheria yote.

4. Kama mnatazamia kufanywa waadilifu kwa njia ya sheria, basi, mmejitenga mbali na Kristo; mko nje ya neema ya Mungu.

5. Kwa upande wetu, lakini, sisi tunangojea kwa matumaini kwa nguvu ya Roho tufanywe waadilifu kwa njia ya imani.

6. Maana ikiwa tumeungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutotahiriwa hakuna maana; cha maana ni imani ifanyayo kazi kwa mapendo.

7. Mwenendo wenu ulikuwa mzuri! Nani, basi, aliyewazuia kuuzingatia ukweli?

8. Aliyesababisha hali hiyo si Mungu ambaye amewaiteni.

9. “Chachu kidogo tu huchachusha donge lote la unga!”

Kusoma sura kamili Wagalatia 5