Agano la Kale

Agano Jipya

Wagalatia 1:18-24 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.

19. Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.

20. Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.

21. Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.

22. Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.

23. Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: “Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza.”

24. Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

Kusoma sura kamili Wagalatia 1