Agano la Kale

Agano Jipya

Wagalatia 1:17-24 Biblia Habari Njema (BHN)

17. na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.

18. Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.

19. Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.

20. Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.

21. Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.

22. Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.

23. Walichokuwa wanajua ni kile tu walichosikia: “Mtu yule aliyekuwa akitutesa hapo awali, sasa anaihubiri imani ileile aliyokuwa anajaribu kuiangamiza.”

24. Basi, wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

Kusoma sura kamili Wagalatia 1