Agano la Kale

Agano Jipya

Wagalatia 1:15-22 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Lakini Mungu, kwa neema yake, alikuwa ameniteua hata kabla sijazaliwa, akaniita nimtumikie.

16. Mara tu alipoamua kunifunulia Mwanawe kusudi niihubiri Habari Njema yake kwa watu wa mataifa mengine, bila kutafuta maoni ya binadamu,

17. na bila kwenda kwanza Yerusalemu kwa wale waliopata kuwa mitume kabla yangu, nilikwenda kwanza Arabia, kisha nikarudi tena Damasko.

18. Ilikuwa tu baada ya miaka mitatu, ndipo nilipokwenda Yerusalemu kuonana na Kefa; nilikaa kwake siku kumi na tano.

19. Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.

20. Haya ninayowaandikieni, Mungu anajua; sisemi uongo.

21. Baadaye nilikwenda katika tarafa za Siria na Kilikia.

22. Wakati huo, mimi binafsi sikujulikana kwa jumuiya za Wakristo kule Yudea.

Kusoma sura kamili Wagalatia 1