Agano la Kale

Agano Jipya

Waefeso 6:21-24 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Tukiko, ndugu yetu mpenzi na mtumishi mwaminifu katika kuungana na Bwana, atawapeni habari zangu zote mpate kujua ninachofanya.

22. Namtuma kwenu awapeni habari zetu mpate kuwa na moyo.

23. Ninawatakieni nyinyi ndugu amani, upendo na imani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Bwana Yesu Kristo.

24. Nawatakia neema ya Mungu wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa mapendo yasiyo na mwisho.

Kusoma sura kamili Waefeso 6