Agano la Kale

Agano Jipya

Waefeso 5:15-20 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi. Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.

16. Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.

17. Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.

18. Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.

19. Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na Zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.

20. Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.

Kusoma sura kamili Waefeso 5