Agano la Kale

Agano Jipya

Tito 2:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho sahihi.

2. Waambie wanaume wazee kwamba wanapaswa kuwa na kiasi, wawe na busara na wataratibu; wanapaswa kuwa timamu katika imani yao, upendo na uvumilivu.

3. Hali kadhalika waambie wanawake wazee wawe na mwenendo wa uchaji wa Mungu; wasiwe wachongezi au watumwa wa pombe. Wanapaswa kufundisha mambo mema,

4. ili wawazoezeshe kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto,

5. wawe na kiasi na safi, waangalie vizuri mambo ya nyumbani, na wawatii waume zao, ili ujumbe wa Mungu usije ukadharauliwa.

6. Kadhalika, wahimize vijana wawe na kiasi.

7. Katika mambo yote wewe mwenyewe unapaswa kuwa mfano wa matendo mema. Uwe mnyofu na uwe na uzito katika mafundisho yako.

Kusoma sura kamili Tito 2