Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 28:2-5 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Ghafla kukatokea tetemeko kubwa la nchi; malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akalivingirisha lile jiwe, akalikalia.

3. Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.

4. Walinzi wa lile kaburi wakatetemeka kwa hofu kubwa, hata wakawa kama wamekufa.

5. Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, “Nyinyi msiogope! Najua kwamba mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.

Kusoma sura kamili Mathayo 28