Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 28:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Na kama mkuu wa mkoa akijua jambo hili, sisi tutasema naye na kuhakikisha kuwa nyinyi hamtapata matatizo.”

15. Wale walinzi wakazichukua zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Habari hiyo imeenea kati ya Wayahudi mpaka leo.

16. Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya kwenye ule mlima aliowaagizia Yesu.

17. Walipomwona wakamwabudu, ingawa wengine walikuwa na mashaka.

18. Yesu akaja karibu, akawaambia, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

19. Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.

20. Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati.”

Kusoma sura kamili Mathayo 28