Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 27:63-66 Biblia Habari Njema (BHN)

63. Wakasema, “Mheshimiwa, tunakumbuka kwamba yule mdanganyifu alisema kabla ya kufa ati, ‘Baada ya siku tatu nitafufuka.’

64. Kwa hiyo amuru kaburi lilindwe mpaka siku ya tatu ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kuwaambia watu kwamba amefufuka. Uongo huu wa mwisho utakuwa mbaya zaidi kuliko ule wa awali.”

65. Pilato akawaambia, “Haya, mnao walinzi; nendeni mkalinde kadiri mjuavyo.”

66. Basi, wakaenda, wakalilinda kaburi, wakatia mhuri juu ya lile jiwe na kuacha hapo askari walinzi.

Kusoma sura kamili Mathayo 27