Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 27:32-36 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Walipokuwa wakienda, wakamkuta mtu mmoja jina lake Simoni, mwenyeji wa Kurene, wakamlazimisha kuuchukua msalaba wake Yesu.

33. Walipofika mahali paitwapo Golgotha, maana yake, mahali pa Fuvu la Kichwa,

34. wakampa mchanganyiko wa divai na kitu kichungu. Lakini Yesu alipoonja akakataa kunywa.

35. Walimsulubisha, kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.

36. Wakaketi, wakawa wanamchunga.

Kusoma sura kamili Mathayo 27