Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 27:26-30 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Hapo Pilato akawafungulia Baraba kutoka gerezani, na baada ya kumpiga Yesu mijeledi, akamtoa asulubiwe.

27. Kisha askari wa mkuu wa mkoa wakamwingiza Yesu ndani ya ikulu, wakamkusanyikia kikosi kizima.

28. Wakamvua nguo zake, wakamvika joho la rangi nyekundu.

29. Kisha wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani, wakamwekea pia mwanzi katika mkono wake wa kulia. Wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki wakisema, “Shikamoo mfalme wa Wayahudi!”

30. Wakamtemea mate, wakauchukua ule mwanzi, wakampiga nao kichwani.

Kusoma sura kamili Mathayo 27