Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 26:65-74 Biblia Habari Njema (BHN)

65. Hapo, kuhani mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.

66. Nyinyi mwaonaje?” Wao wakamjibu, “Anastahili kufa!”

67. Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,

68. wakasema, “Tubashirie basi, wewe Kristo; ni nani amekupiga!”

69. Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, “Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”

70. Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”

71. Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”

72. Petro akakana tena kwa kiapo: “Simjui mtu huyo.”

73. Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha.”

74. Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, “Simjui mtu huyo!” Mara jogoo akawika.

Kusoma sura kamili Mathayo 26