Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 26:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,

2. “Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe.”

3. Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, kuhani mkuu.

4. Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.

5. Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.

6. Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,

7. mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.

8. Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Ya nini hasara hii?

9. Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha.”

10. Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.

11. Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.

12. Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.

Kusoma sura kamili Mathayo 26