Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 24:41-51 Biblia Habari Njema (BHN)

41. Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.

42. Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.

43. Lakini kumbukeni jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.

44. Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”

45. Yesu akaendelea kusema, “Ni nani basi mtumishi mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watu wake, awape chakula kwa wakati wake?

46. Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.

47. Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.

48. Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: ‘Bwana wangu amekawia kurudi,’

49. kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,

50. bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.

51. Atamwadhibu vibaya na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.

Kusoma sura kamili Mathayo 24