Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 24:13-24 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.

14. Ila, kabla ya mwisho kufika, hii Habari Njema ya ufalme wa Mungu itahubiriwa ulimwenguni kote kama ushuhuda kwa mataifa yote.

15. “Basi, mtakapoona ‘Chukizo Haribifu lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu, (msomaji na atambue maana yake),

16. hapo, walioko Yudea na wakimbilie milimani.

17. Aliye juu ya paa la nyumba yake asishuke kuchukua kitu nyumbani mwake.

18. Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.

19. Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!

20. Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe siku za baridi au siku ya Sabato!

21. Maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka leo, wala haitapata kutokea tena.

22. Kama siku hizo hazingalipunguzwa, hakuna binadamu yeyote ambaye angeokoka; lakini siku hizo zitapunguzwa kwa ajili ya wale walioteuliwa.

23. “Basi, mtu akiwaambieni siku hizo: ‘Kristo yuko hapa’ au ‘Yuko pale,’ msimsadiki.

24. Maana watatokea akina Kristo wa uongo na manabii wa uongo. Watafanya ishara kubwa na maajabu ya kuweza kuwapotosha ikiwezekana hata wateule wa Mungu.

Kusoma sura kamili Mathayo 24