Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 21:5-11 Biblia Habari Njema (BHN)

5. “Uambieni mji wa Siyoni:Tazama, Mfalme wako anakujia!Ni mpole na amepanda punda,mwanapunda, mtoto wa punda.”

6. Hivyo, wale wanafunzi walikwenda wakafanya kama Yesu alivyowaagiza.

7. Wakamleta yule punda na mtoto wake, wakatandika nguo zao juu yao na Yesu akaketi juu yake.

8. Umati mkubwa wa watu wakatandaza nguo zao barabarani, na watu wengine wakakata matawi ya miti wakayatandaza barabarani.

9. Makundi ya watu waliomtangulia na wale waliomfuata wakapaza sauti:“Sifa kwa Mwana wa Daudi!Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana!Sifa kwa Mungu juu!”

10. Yesu alipokuwa anaingia Yerusalemu, mji wote ukajaa ghasia. Watu wakawa wanauliza, “Huyu ni nani?”

11. Watu katika ule umati wakasema, “Huyu ni nabii Yesu, kutoka Nazareti mji wa Galilaya.”

Kusoma sura kamili Mathayo 21