Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 21:39-46 Biblia Habari Njema (BHN)

39. Basi, wakamkamata, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamuua.

40. “Sasa, huyo mwenye shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanyaje hao wakulima?”

41. Wao wakamjibu, “Atawaangamiza vibaya hao waovu, na lile shamba atawapa wakulima wengine ambao watampa sehemu ya mavuno wakati wake.”

42. Hapo Yesu akawaambia, “Je, hamkusoma jambo hili katika Maandiko Matakatifu?‘Jiwe walilokataa waashisasa limekuwa jiwe kuu la msingi.Bwana ndiye aliyefanya jambo hili,nalo ni la ajabu sana kwetu!’

43. “Kwa hiyo nawaambieni, ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu na kupewa watu wa mataifa mengine wenye kutoa matunda yake.”

44. Atakayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamponda” (taz. Luka 20:18).

45. Makuhani wakuu na Mafarisayo waliposikia hiyo mifano yake walitambua kwamba alikuwa anawasema wao.

46. Kwa hiyo wakawa wanatafuta njia ya kumtia nguvuni, lakini waliwaogopa watu kwa sababu wao walimtambua yeye kuwa nabii.

Kusoma sura kamili Mathayo 21