Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 21:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yesu na wanafunzi wake walipokaribia Yerusalemu na kufika Bethfage katika mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,

2. akawaambia, “Nendeni hadi kijiji kilicho mbele yenu na mtamkuta punda amefungwa na mtoto wake. Wafungueni mkawalete kwangu.

3. Kama mtu akiwauliza sababu, mwambieni, ‘Bwana anawahitaji,’ naye atawaachieni mara.”

4. Jambo hili lilifanyika ili yale yaliyosemwa na nabii yatimie:

5. “Uambieni mji wa Siyoni:Tazama, Mfalme wako anakujia!Ni mpole na amepanda punda,mwanapunda, mtoto wa punda.”

Kusoma sura kamili Mathayo 21