Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 11:4-10 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Yesu akawajibu, “Nendeni mkamwambie Yohane mambo mnayoyasikia na kuyaona:

5. Vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa Habari Njema.

6. Heri mtu yule ambaye hana mashaka nami.”

7. Basi, hao wajumbe wa Yohane walipokuwa wanakwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu habari za Yohane: “Mlikwenda kutazama nini kule jangwani? Je, mlitaka kuona mwanzi unaotikiswa na upepo?

8. Basi, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona mtu aliyevaa mavazi maridadi? Watu wanaovaa mavazi maridadi hukaa katika nyumba za wafalme.

9. Lakini, mlikwenda kuona nini? Nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.

10. “Huyu ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu:‘Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu akutangulie,ambaye atakutayarishia njia yako’.

Kusoma sura kamili Mathayo 11