Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 11:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Kama mwaweza kukubali basi, Yohane ndiye Elia ambaye angekuja.

15. Mwenye masikio na asikie!

16. “Basi, nitakifananisha kizazi hiki na kitu gani? Ni kama vijana waliokuwa wamekaa uwanjani, wakawa wakiambiana kikundi kimoja kwa kingine:

17. ‘Tumewapigieni ngoma lakini hamkucheza!Tumeimba nyimbo za huzuni lakini hamkuomboleza!’

18. Kwa maana Yohane alikuja, akafunga na wala hakunywa divai, nao wakasema: ‘Amepagawa na pepo’.

19. Mwana wa Mtu akaja, anakula na kunywa, nao wakasema: ‘Mwangalieni huyu, mlafi na mlevi, rafiki yao watozaushuru na wenye dhambi!’ Hata hivyo, hekima ya Mungu inathibitishwa kuwa njema kutokana na matendo yake.”

20. Kisha Yesu akaanza kuilaumu miji ambayo, ingawaje alifanya miujiza mingi humo, watu wake hawakutaka kutubu:

Kusoma sura kamili Mathayo 11