Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 10:3-11 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Filipo na Bartholomayo, Thoma na Mathayo aliyekuwa mtozaushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;

4. Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.

5. Yesu aliwatuma hao kumi na wawili na kuwapa maagizo haya: “Msiende kwa watu wa mataifa mengine, wala msiingie katika miji ya Wasamaria.

6. Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.

7. Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’

8. Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.

9. Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.

10. Msichukue mkoba wa kuombea njiani, wala koti la ziada, wala viatu, wala fimbo. Maana mfanyakazi anastahili riziki yake.

11. “Mkiingia katika mji wowote au kijiji, tafuteni humo mtu anayestahili kutembelewa, na kaeni huko mpaka mtakapoondoka mahali hapo.

Kusoma sura kamili Mathayo 10