Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 10:28-32 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Afadhali zaidi kumwogopa yule awezaye kuuangamiza mwili pamoja na roho katika moto wa Jehanamu.

29. Shomoro wawili huuzwa kwa sarafu moja ndogo. Lakini hata mmoja wao haanguki chini bila kibali cha Baba yenu.

30. Lakini kwa upande wenu, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.

31. Kwa hiyo msiogope; nyinyi mna thamani kuliko shomoro wengi.

32. “Kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, mimi pia nitamkiri mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.

Kusoma sura kamili Mathayo 10