2. Majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya: Wa kwanza ni Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohane ndugu yake;
3. Filipo na Bartholomayo, Thoma na Mathayo aliyekuwa mtozaushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;
4. Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
5. Yesu aliwatuma hao kumi na wawili na kuwapa maagizo haya: “Msiende kwa watu wa mataifa mengine, wala msiingie katika miji ya Wasamaria.
6. Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.
7. Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’
8. Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.
9. Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.