Agano la Kale

Agano Jipya

Mathayo 10:2-9 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya: Wa kwanza ni Simoni aitwaye Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohane ndugu yake;

3. Filipo na Bartholomayo, Thoma na Mathayo aliyekuwa mtozaushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;

4. Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.

5. Yesu aliwatuma hao kumi na wawili na kuwapa maagizo haya: “Msiende kwa watu wa mataifa mengine, wala msiingie katika miji ya Wasamaria.

6. Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.

7. Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’

8. Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.

9. Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.

Kusoma sura kamili Mathayo 10