Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 8:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.

5. Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.

6. Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.

7. Maana pepo wachafu waliokuwa wamewapagaa watu wengi waliwatoka wakipiga kelele kubwa; na pia watu wengi waliokuwa wamepooza viungo na waliolemaa waliponywa.

8. Kukawa na furaha kubwa katika mji ule.

Kusoma sura kamili Matendo 8