Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 8:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Saulo naye alikiona kitendo hicho cha kumwua kuwa sawa.Siku hiyo kanisa la Yerusalemu lilianza kuteswa vibaya. Waumini wote, isipokuwa tu wale mitume, walilazimika kutawanyika katika sehemu za mashambani za Yudea na Samaria.

2. Watu wamchao Mungu walimzika Stefano na kumfanyia maombolezo makubwa.

3. Wakati huohuo, Saulo alijaribu kuliangamiza kanisa. Alikwenda katika kila nyumba, akawatoa nje waumini, wanaume kwa wanawake, akawatia gerezani.

4. Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.

5. Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.

6. Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.

Kusoma sura kamili Matendo 8