Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 7:41-46 Biblia Habari Njema (BHN)

41. Hapo ndipo walipojitengenezea sanamu ya ndama, wakaitambikia na kukifanyia sherehe kitu ambacho ni kazi ya mikono yao wenyewe.

42. Lakini Mungu aliondoka kati yao, akawaacha waabudu nyota za anga, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii:‘Enyi watu wa Israeli!Si mimi mliyenitolea tambiko na sadakakwa miaka arubaini kule jangwani!

43. Nyinyi mlikibeba kibanda cha mungu Moloki,na sanamu ya nyota ya mungu wenu Refani.Sanamu mlizozifanya ndizo mlizoabudu.Kwa sababu hiyo nitawapeleka mateka mbali kupita Babuloni!’

44. Kule jangwani babu zetu walikuwa na lile hema la maamuzi. Lilitengenezwa kama Mungu alivyomwambia Mose alifanye; nakala kamili ya kile alichooneshwa.

45. Kisha babu zetu walilipokezana wao kwa wao mpaka wakati wa Yoshua, walipoinyakua ile nchi kutoka kwa mataifa ambayo Mungu aliyafukuza mbele yao. Hapo lilikaa mpaka nyakati za Daudi.

46. Daudi alipata upendeleo kwa Mungu, akamwomba Mungu ruhusa ya kumjengea makao yeye aliye Mungu wa Yakobo.

Kusoma sura kamili Matendo 7