Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 7:18-25 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Mwishowe, mfalme mmoja ambaye hakumtambua Yosefu alianza kutawala huko Misri.

19. Alilifanyia taifa letu ukatili, akawatendea vibaya babu zetu kwa kuwalazimisha waweke nje watoto wao wachanga ili wafe.

20. Mose alizaliwa wakati huo. Alikuwa mtoto mzuri sana. Alilelewa nyumbani kwa muda wa miezi mitatu,

21. na alipotolewa nje, binti wa Farao alimchukua, akamlea kama mtoto wake.

22. Mose alifundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri akawa mashuhuri kwa maneno na matendo.

23. “Alipokuwa na umri wa miaka arubaini aliamua kwenda kuwaona ndugu zake Waisraeli.

24. Huko alimwona mmoja wao akitendewa vibaya, akaenda kumwokoa, na kwa kulipiza kisasi, akamuua yule Mmisri. (

25. Alidhani kwamba Waisraeli wenzake wangeelewa kwamba Mungu angemtumia yeye kuwakomboa, lakini hawakuelewa hivyo).

Kusoma sura kamili Matendo 7