Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 4:24-29 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Nao waliposikia habari hizo waliungana pamoja katika kumwomba Mungu wakisema, “Bwana, wewe ni Muumba wa mbingu na dunia, bahari na vyote vilivyomo!

25. Ndiwe uliyemfanya mtumishi wako, baba yetu Daudi, aseme kwa nguvu ya Roho Mtakatifu:‘Kwa nini mataifa yameghadhibika?Mbona watu wamefanya mipango ya bure?

26. Wafalme wa dunia walijiweka tayari,na watawala walikutana pamoja,dhidi ya Bwana na dhidi ya Kristo wake.’

27. “Maana, kwa hakika, ndivyo Herode, Pontio Pilato, watu wa Israeli na watu wa mataifa walivyokutanika papa hapa mjini, kumpinga Yesu Mtumishi wako Mtakatifu ambaye ulimweka wakfu.

28. Naam, walikutana ili wafanye mambo yale uliyokusudia na kupanga tangu mwanzo kwa uwezo wako na mapenzi yako.

29. Lakini sasa, ee Bwana, angalia vitisho vyao. Utuwezeshe sisi watumishi wako kuhubiri neno lako kwa uhodari.

Kusoma sura kamili Matendo 4