Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 28:27-31 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Maana akili za watu hawa zimepumbaa,wameziba masikio yao,wamefumba macho yao.La sivyo, wangeona kwa macho yao,wangesikia kwa masikio yao.Wangeelewa kwa akili zao,na kunigeukia, asema Bwana,nami ningewaponya.’”

28. Halafu Paulo akasema, “Jueni basi, kwamba ujumbe wa Mungu juu ya wokovu umepelekwa kwa watu wa mataifa. Wao watasikiliza!” [

29. Paulo alipokwisha sema hayo, Wayahudi walijiondokea huku wakiwa wanabishana vikali wao kwa wao.]

30. Kwa muda wa miaka miwili mizima Paulo aliishi katika nyumba aliyoipanga yeye mwenyewe; akawa anawakaribisha wote waliofika kumsalimu.

31. Alikuwa akihubiri ufalme wa Mungu na kufundisha juu ya Bwana Yesu Kristo kwa uhodari, bila kizuizi.

Kusoma sura kamili Matendo 28