Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 19:9-11 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Lakini wengine walikuwa wakaidi, wakakataa kuamini, wakaanza kuongea vibaya juu ya hiyo njia ya Bwana katika kusanyiko la watu. Hapo Paulo alivunja uhusiano nao, akawachukua pembeni wale wanafunzi wake, akawa anazungumza nao kila siku katika jumba la masomo la Turano.

10. Aliendelea kufanya hivyo kwa muda wa miaka miwili hata wakazi wote wa Asia, Wayahudi na watu wa mataifa mengine, wakaweza kusikia neno la Bwana.

11. Mungu alifanya miujiza ya ajabu kwa mikono ya Paulo.

Kusoma sura kamili Matendo 19