Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 17:28-31 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Kama alivyosema mtu mmoja:‘Ndani yake yeye sisi tunaishi,tunajimudu, na tuko!’Ni kama washairi wenu wengine walivyosema:‘Sisi ni watoto wake.’

29. Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.

30. Mungu alifanya kana kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.

31. Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka kwa wafu!”

Kusoma sura kamili Matendo 17