Agano la Kale

Agano Jipya

Matendo 15:31-35 Biblia Habari Njema (BHN)

31. Walipoisoma hiyo barua, maneno yake yaliwatia moyo, wakafurahi sana.

32. Yuda na Sila, ambao nao walikuwa manabii, walizungumza na hao ndugu kwa muda mrefu wakiwatia moyo na kuwaimarisha.

33. Baada ya kukaa huko kwa muda fulani, ndugu wa Antiokia waliwaaga wakiwatakia amani, kisha wakarudi kwa wale waliokuwa wamewatuma. [

34. Lakini Sila aliamua kubaki.]

35. Paulo na Barnaba walibaki huko Antiokia kwa muda; wakafundisha na kuhubiri neno la Bwana, pamoja na watu wengine wengi.

Kusoma sura kamili Matendo 15